Kutokana na mafuriko makubwa yaliyotokea hivi karibuni wilayani kyela, wakazi wengi wamejikuta hawana uhakika wa kujipatia chakula, mahala pa kulala, Mavazi ya kuvaa wala uhakika kuendelea kufanya shughuli zao za kiuchumi na Kupelekea hali kuwa tete zaidi.
waathirika wakubwa wa adha hizi ni kundi la watoto na wanawake.
waathirika wakubwa wa adha hizi ni kundi la watoto na wanawake.
baadhi ya wanachi waliokosa makazi baaada ya makazi yao kuingiliwa na mafuriko
wananchi wenye mapenzi mema na moyo wa huruma wanaombwa kujitolea kuwasaidia wahanga hawa kwa chochote, kama Vyakula, Mavazi na fedha.
kwa upande wa mkoa wa mbeya shughuli za ukusanyaji wa misaada kwa ajiri ya wahanga hawa zinaendeshwa na Taasisi ya Muungano wa Jamii Tanzania (MUJTA) ikishirikiana na Red Cross na skauti.
zoezi la ukusanyaji wa misaada hii litaanza tarehe 28 / 05 / 2014. na wakusanyaji watapita maeneo mbali mbali wakiwa wamevalia mavazi ya red cros, Mashat ya MUJATA ama watakuwa na vitambulisho vya mujata.
watanzania mnaombwa ushirikano wenu ili kuweza kuwakwamua ndugu zetu hawa kama ilivyo desturi yetu watanzania ya kupendana na kusaidiana
baadhi ya maeneo ya makazi ya watu yaliyoingiliwa na maji
vituo maalum vya ukusanyaji wa misaada hiyo vitatajwa kupaitia redia zote za mbeya ama kupitia blog hii. na namba za simu kwa ajiri ya kutuma pesa zitatajwa pia redioni humo
maeneo mengine ya barabara na mashamba yaliyokumbwa na mafuriko wilayani kyela