Sunday 11 May 2014

Waganga wa Jadi watahadharishwa kutumia Alama ya Msalaba Mwekundu

Na Stephano Simbeye,

Chama Cha Msalaba mwekundu kimewatahadharisha waganga wa jadi pamoja na taasisi zingine zinazotumia Alama ya msalaba Mwekundu katika shughuli zao kuwa ni makosa na ni kinyume na sheria.

Tahadhari hii ilitolewa na Makamu wa raisi wa chama hicho Dr. Zainabu Gama alipokuwa akihutubia katika kilele cha sherehe za maadhimisho ya siku ya msalaba mwekundu duniani zilizofanyikia kitaifa mkoani mbeya katika viwanja vya Rwanda Nzovwe.

Dr. Zainabu alisema kuwa kumekuwa na matumizi holela ya alama ya Msalaba mwekundu ambapo nembo hiyo inatumiwa na baadhi ya waganga wa jadi katika shughuli zao ikiwamo na baadi ya taasisi zingine amabazo hazina uhusiano kabisa na chama cha msalaba mwekundu.
Aliziweka wazi taasisi zingine zinazotumia alama hiyo kimakosa kuwa ni pamoja na hospitari na magari ya kubebea wagonjwa.
                                  
Alama ya msalaba inayotumiwa na Chama Cha Msalaba Mwekundu (picha kutoka mtandaoni)

Dr. Zainabu alitoa msisitizo kuwa matumizi holela ya nembo hiyo ni kinyume na sheria ya mwaka 1962 iliyoundwa na chama cha msalaba mwekundu ambayo kwa sasa inafanyiwa marekebisho na bunge inayoruhusu alama ya msalaba mwekundu kutumiwa na chama cha msalaba mwekundu na sehemu ya jeshi  tu ambayo ndiyo inayotoa huduma za kiafya katika chama hicho.

“Naiomba serikari kuchukua hatua za haraka kurekebisha sheria ya msalaba mwekundu ili kuweza kudhibiti matumizi holela ya nembo hiyo” alisema Dr. Zainabu

Kwa upande wake mgeni rasmi wa sherehe hizo kutoka Wizara ya Afya Bw. Deodatus Kinawilo alidhibitisha kutumika kwa alama ya msalaba mwekundu katika shughuli za hospitali za serikali pamoja na magari ya kubebea wagonjwa na aliahidi kutafuta namna ya kuweza kalitatua swala hilo.

Aidha Dr. Zainabu alitoa ufafanuzu juu ya utofauti uliopo kati ya alama ya msalaba inayotumiwa na chama cha msalaba mwekundu na ile inayotumiwa makanisani kuwa  alama ya msalaba inayotumiwa na chama cha msalaba mwekundu ina nguo mbili zenye urefu sawa wakati nembo inayotumiwa makanisani ina nguzo msimamo ambayo ni ndefu zaidi ya nguzo mlalo.

Alama ya Msalaba inayotumiwa Makanisani (picha toka mtandaoni)